Masaa kadhaa baada ya Al Ahly kususia mchezo wake wa dabi dhidi ya Zamalek kwa kigezo cha kukiukwa kwa makubaliano baina ya Shirikisho la soka la Misiri na wao lakuleta marefa wa kigeni kuchezesha mchezo huo, hali imekuwa tofauti kwa Zamalek ambaye hakugomea mchezo huo na kuishia kupewa ushindi wa mezani wa alama 3 na magoli matatu.
Al Ahly alibakia na msimamo wake wakutokwenda uwanjani na kutoshiriki mchezo huo licha ya kuombwa kushiriki. Al Ahly imetangaza kurudisha pesa kwa mashabiki zake walionunua tiketi kwaajili ya mchezo huo.
Baada ya Zamalek kupewa alama 3 za mezani Al Ahly hawajatoa tamko lolote mpaka sasa huku wengi wakisubiri kuona nini maamuzi yao maana awali walitishia kujitoa kwenye ligi iwapo waamuzi wa kigeni hawatachezesha mchezo huo.