José Luis Munuera Montero, mwamuzi wa ligi kuu ya Uhispania aliyempa kadi nyekundu Jude Bellingham wa Real Madrid katika sare ya 1-1 dhidi ya Osasuna hivi karibuni, amesema amepokea vitisho na matusi kwake na familia yake hivi karibuni kufuatia Kadi nyekundu hiyo ilitolewa kwa madai ya lugha ya matusi iliyotolewa dhidi yake wakati wa mchezo.
Kutokana na vitisho na matusi aliyopokea baada ya tukio hilo, Shirikisho la Soka la Hispania (RFEF) limetoa taarifa likilaani vitendo hivyo na kuonyesha kumuunga mkono mwamuzi huyo.
Zaidi ya hayo, Montero kwa sasa anachunguzwa na RFEF kwa madai ya mgongano wa maslahi kutokana na ushiriki wake katika Talentus Sports, kampuni ya ushauri wa michezo. Ameshikiliwa mbali na majukumu yake ya uamuzi wa mechi hadi uchunguzi utakapokamilika.
Hadi sasa, Montero hajatoa kauli yoyote ya umma kuhusu tukio la kadi nyekundu kwa Bellingham au uchunguzi unaoendelea kuhusu shughuli zake za Uamuzi.