Mahakama ya Kijeshi Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imetoa hati ya kukamatwa kiongozi wa waasi

Mahakama ya kijeshi katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imetoa hati ya kimataifa ya kukamatwa kwa kiongozi wa Muungano wa Mto Kongo (Congo River Alliance), ambao unajumuisha kundi la waasi la M23, kwa mashtaka ya uhalifu wa kivita na usaliti.

Vyombo vya habari vya serikali viliripoti siku ya Alhamisi kwamba hati hiyo ya kukamatwa ilitolewa Jumanne dhidi ya Corneille Nangaa kwa mauaji ya kimbari anayotuhumiwa kuyafanya katika jimbo la Kivu Kaskazini na, hivi karibuni, Kivu Kusini, yote ikiwa ni maeneo ya mashariki mwa DRC. Matendo haya yanachukuliwa kuwa uhalifu chini ya sheria za Kongo na sheria za kimataifa. Mahakama imeamuru Nangaa akamatwe popote alipo ili ashtakiwe katika ardhi ya Kongo.

Ghasia zilianza katika mji wa Goma, ambao una watu milioni mbili, mashariki mwa DRC, wiki mbili zilizopita wakati wapiganaji wa M23 walipoanzisha mashambulizi makubwa dhidi ya vikosi vya serikali. Siku ya Jumatano, Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Masuala ya Kibinadamu ilikadiria kuwa takriban watu 2,800 wamekufa mjini Goma kutokana na ghasia hizo.

Maelfu ya watu pia wamelazimika kuhama makazi yao, wengi wakikimbilia nchi jirani ya Rwanda, wakiwemo wafanyakazi wa mashirika ya kimataifa kama Umoja wa Mataifa na Benki ya Dunia.

Shirika la Misaada la Kanisa la Uswisi (Swiss Church Aid) liliripoti siku ya Alhamisi kwamba wafanyakazi wake watatu wa ndani waliuawa katika shambulio lililotokea kwenye eneo la Rutshuru, ambalo lilitekwa na wapiganaji wa M23 wiki iliyopita. Shirika hilo, linalojulikana pia kama HEKS/EPER, halikubainisha ni nani aliyewajibika kwa vifo hivyo.

Siku ya Jumatatu, M23 ilitangaza kusitisha mapigano baada ya kupigana na jeshi la Kongo kwa ajili ya udhibiti wa Goma. Hata hivyo, siku ya Jumatano, kundi hilo liliteka mji wa Nyabibwe, eneo la uchimbaji madini katika jimbo la Kivu Kusini, hatua inayoonekana kuwa uvunjaji wa usitishaji mapigano walioutangaza wenyewe.

Mshirikishe Mwingine

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Mahakama ya Kijeshi Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imetoa hati ya kukamatwa kiongozi wa waasi

Mahakama ya kijeshi katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imetoa hati ya kimataifa ya kukamatwa kwa kiongozi wa Muungano wa Mto Kongo (Congo River Alliance), ambao unajumuisha kundi la waasi la M23, kwa mashtaka ya uhalifu wa kivita na usaliti.

Vyombo vya habari vya serikali viliripoti siku ya Alhamisi kwamba hati hiyo ya kukamatwa ilitolewa Jumanne dhidi ya Corneille Nangaa kwa mauaji ya kimbari anayotuhumiwa kuyafanya katika jimbo la Kivu Kaskazini na, hivi karibuni, Kivu Kusini, yote ikiwa ni maeneo ya mashariki mwa DRC. Matendo haya yanachukuliwa kuwa uhalifu chini ya sheria za Kongo na sheria za kimataifa. Mahakama imeamuru Nangaa akamatwe popote alipo ili ashtakiwe katika ardhi ya Kongo.

Ghasia zilianza katika mji wa Goma, ambao una watu milioni mbili, mashariki mwa DRC, wiki mbili zilizopita wakati wapiganaji wa M23 walipoanzisha mashambulizi makubwa dhidi ya vikosi vya serikali. Siku ya Jumatano, Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Masuala ya Kibinadamu ilikadiria kuwa takriban watu 2,800 wamekufa mjini Goma kutokana na ghasia hizo.

Maelfu ya watu pia wamelazimika kuhama makazi yao, wengi wakikimbilia nchi jirani ya Rwanda, wakiwemo wafanyakazi wa mashirika ya kimataifa kama Umoja wa Mataifa na Benki ya Dunia.

Shirika la Misaada la Kanisa la Uswisi (Swiss Church Aid) liliripoti siku ya Alhamisi kwamba wafanyakazi wake watatu wa ndani waliuawa katika shambulio lililotokea kwenye eneo la Rutshuru, ambalo lilitekwa na wapiganaji wa M23 wiki iliyopita. Shirika hilo, linalojulikana pia kama HEKS/EPER, halikubainisha ni nani aliyewajibika kwa vifo hivyo.

Siku ya Jumatatu, M23 ilitangaza kusitisha mapigano baada ya kupigana na jeshi la Kongo kwa ajili ya udhibiti wa Goma. Hata hivyo, siku ya Jumatano, kundi hilo liliteka mji wa Nyabibwe, eneo la uchimbaji madini katika jimbo la Kivu Kusini, hatua inayoonekana kuwa uvunjaji wa usitishaji mapigano walioutangaza wenyewe.

Mshirikishe Mwingine

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *