Rapa Joyner Lucas ameweka wazi nia yake yakurudi kwenye mashindano ya rap baada ya kuandika kwenye mtandao wa X matamanio yake.
“Wakati mwingine najikuta natamani kurudi kwenye ulingo wa URL battle rap” aliandika hivyo.
URL ( Ultimate Rap League) walijubu nukuu yake kwa kuonyesha utayari wao wakisema “Tufanye kazi hiyo”.
Aidha matamanio yake awali yalikuwa kupambana na yeyote atakayependekezwa na URL ila Joyner aliamua kuweka pendekezo lake na kumtaja Rapa Meek Mill kuwa angepende awe mshindani wake.
Mashabiki wanasubiri kuona kama Meek Mill atajibu hii na kama battle rap itafanyika.