Vatican imeeleza kuwa kiongozi wa kanisa la katoliki duniani, Papa Francis hayuko tena kwenye hatari ya kifo kutokana na maradhi yanayomsumbua.
Imeelezwa kuwa dawa anazotumia Papa Francis zimeanza kuleta matokeo chanya kwenye mwili wake. Hali ya maendeleo ya kuimarika kwa afya ya kiongozi huyo imeonekana jana kwenye mfumo wa mapafu yake.
Ni wiki tatu tangu Papa Francis alazwe katika hospitali ya Gemelli mjini Roma. Taarifa zilidai anasumbuliwa na maambukizi makali kwenye mfumo wa upumuaji ambayo yamewalazimu madaktari wanaomtibu kumuweka katika uangalizi wa karibu kulinda afya yake.