DeepSeek kampuni mpya ya AI China yashusha hisa kampuni za teknolojia Marekani

Hisa kubwa za teknolojia za Marekani ikiwemo Nvidia, Microsoft, na Tesla zilipoteza thamani ya dola trilioni 1 siku ya Jumatatu, kutokana na hofu kuhusu mfano wa hali ya juu wa akili bandia (AI) kutoka China, hali iliyosababisha mshituko kutoka Wall Street hadi Silicon Valley.

Kampuni ya kutengeneza chipu ya Nvidia, ambayo iliongoza kwa AI mwaka jana na kuwa kampuni tajiri zaidi duniani, ilishuka kwa karibu 17% ikipoteza thamani ya dola bilioni 589 katika anguko kubwa zaidi la siku moja katika historia ya soko baada ya wawekezaji kupata habari kuhusu DeepSeek, kampuni ya uanzilishi kutoka China iliyoanzishwa mwezi uliopita tu.

Kuzinduliwa kwa DeepSeek kukitajwa na mwekezaji wa teknolojia Marc Andreessen kama “wakati wa Sputnik wa AI” kumesababisha mshituko wa kimataifa ulioathiri kampuni za AI na watengenezaji wa chipu.

Rais Trump alisema anaiona DeepSeek kama “jambo chanya” na “mwito wa kuamsha sekta zetu kwamba tunahitaji kuwekeza nguvu zetu kushindana na kushinda.”Kampuni hiyo inadai kuwa imeunda chatbot ya hali ya juu ya AI kwa gharama ya chini ya dola milioni 6 na bila kutumia chipu bora zaidi za Nvidia. Hii ni tofauti kubwa na mabilioni ya dola ambayo kwa kawaida hutumiwa na kampuni kubwa za teknolojia za Magharibi kwa utafiti wa AI na utengenezaji wa chipu.

Mshirikishe Mwingine

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

DeepSeek kampuni mpya ya AI China yashusha hisa kampuni za teknolojia Marekani

Hisa kubwa za teknolojia za Marekani ikiwemo Nvidia, Microsoft, na Tesla zilipoteza thamani ya dola trilioni 1 siku ya Jumatatu, kutokana na hofu kuhusu mfano wa hali ya juu wa akili bandia (AI) kutoka China, hali iliyosababisha mshituko kutoka Wall Street hadi Silicon Valley.

Kampuni ya kutengeneza chipu ya Nvidia, ambayo iliongoza kwa AI mwaka jana na kuwa kampuni tajiri zaidi duniani, ilishuka kwa karibu 17% ikipoteza thamani ya dola bilioni 589 katika anguko kubwa zaidi la siku moja katika historia ya soko baada ya wawekezaji kupata habari kuhusu DeepSeek, kampuni ya uanzilishi kutoka China iliyoanzishwa mwezi uliopita tu.

Kuzinduliwa kwa DeepSeek kukitajwa na mwekezaji wa teknolojia Marc Andreessen kama “wakati wa Sputnik wa AI” kumesababisha mshituko wa kimataifa ulioathiri kampuni za AI na watengenezaji wa chipu.

Rais Trump alisema anaiona DeepSeek kama “jambo chanya” na “mwito wa kuamsha sekta zetu kwamba tunahitaji kuwekeza nguvu zetu kushindana na kushinda.”Kampuni hiyo inadai kuwa imeunda chatbot ya hali ya juu ya AI kwa gharama ya chini ya dola milioni 6 na bila kutumia chipu bora zaidi za Nvidia. Hii ni tofauti kubwa na mabilioni ya dola ambayo kwa kawaida hutumiwa na kampuni kubwa za teknolojia za Magharibi kwa utafiti wa AI na utengenezaji wa chipu.

Mshirikishe Mwingine

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *