Waziri Mkuu wa zamani wa Kenya, Rail Odinga amewajia juu wakosoaji wa Serikali ya Rais William Ruto wanaotaka aondoke madarakani huku akisema wanataka atoke aende wapi.
Kauli hiyo imekuja baada ya siku chache nyuma Odinga kusaini makubaliano ya kufanya kazi na Rais William Ruto.
Aidha katika mitandao ya kijamii baadhi ya Wakenya wamekuwa na kauli inayosema “Ruto Must Go” wakimaanisha Rais Ruto lazima aondoke madarakani kauli ambayo Odinga amesema haitasaidia kutatua matatizo na changamoto zinzowakabili Wakenya.