Waziri wa zamani wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Prof. Philemon Sarungi amefariki dunia. Taarifa hii imetolewa na msemaji wa familia Martin Leonard Sarungi.
“Familia ya Chifu Sarungi na ukoo wa.Nyiratho wa Utegi, Rorya, tunasikitika kutangaza kifo cha mpendwa wetu Mzee Profesa Philemon Mikol Sarungi kilichotokea leo tarehe 05/03/2025 saa kumi jioni, msiba upo Oysterbay mtaa wa Msasani Dar es Salaam”.
Taarifa na taratibu zingine kuhusiana na mazishi zitatolewa na familia .