Klabu ya Arsenal imeripotiwa kuhitaji huduma ya mshambuliaji wa RB Leipzig, Benjamin Sesko kwa ajili ya kuimarisha kikosi chao kwenye dirisha lijalo la uhamisho wa majira ya kiangazi.
Arsenal inahitaji mshambuliaji mpya kwenye kikosi chao na hivyo wanamtazama nyota huyo wa kimataifa wa Slovania mwenye umri wa miaka 21 kama chaguo la kwanza kutokana na kiwango chake pia upatikanaji wake ni gharama nafuu.
Miamba hiyo ya Emirates imekuwa na orodha ndefu ya washambuliaji inaowasaka, lakini inamtazama Sesko kuwa nafuu kwao ukilinganisha na mkali wa Newcastle United, Alexander Isak, ambaye ukiweka kando kutakiwa pia na Liverpool, bei yake anayouzwa ni kubwa.