Baadhi ya watumishi kutoka Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), watoa huduma kwa watumiaji na wateja wa mawasiliano katika banda la TCRA, katika maonesho ya Kimataifa ya Biashara, Zanzibar kuelekea kilele cha sherehe za Maadhimisho ya Miaka 61 ya Mapinduzi ya Zanzibar
TCRA ikijumuika na kukaribisha wadau wa sekta ya mawasiliano ili kupata elimu kuhusu historia ya mawasiliano na huduma mbalimbali kuhusu sekta ya mawasiliano huku ikitoa elimu ya matumizi salama ya mitandao kupitia kampeni ya ni rahisi sana inayo eleza urahisi wa kujilinda mitandaoni, kujua taarifa feki, kunufaika na fursa mitandaoni pamoja na kujua utapeli na kuripoti
Akizungumza meneja ofisi ya TCRA Zanzibar Bi. Esuvatie Masunga amewataka wananchi kutumia mawasiliano kulinda amani na kuleta maendeleo sawa na kauli mbiu ya tukio la maadhimisho ya miaka 61 ya mapinduzi Zanzibar
Maonesho hayo yamefanyika katika viwanja vya Nyamanzi, Fumba, na yalianza rasmi tarehe 3 na kuendelea hadi tarehe 12 Januari, 2025.